KAMPEINI ZA PAMBA MOTO TRANS NZOIA KUELEKEA UCHAGUZI WA CHAMA CHA WAFANYIKAZI KAUNTI HIYO.

Zikiwa zimesalia wiki mbili tu kabla uchaguzi wa Chama cha Wafanyakazi wa Kaunti ya Trans Nzoia kufanyika, wawaniaji wa viti mbalimbali wanaendeleza kampeni huku baadhi yao wakiahidi kuboresha mazingira ya utendakazi kupitia mazungumzo na ushauriano na mwajiri.

Mwaniajia wa katibu mkuu wa chama hicho, Ronald Simiyu anasema ilivyo kwa sasa kuna pengo kuu baina ya washikadau hivyo kuchangia mizozo ya kisheria ya mara kwa mara.

Simiyu ambaye ameajiriwa katika kitengo cha kuzima moto na kukabili majanga kunti hiyo amesema atahakikisha kwamba  kila mfanyakazi anawezeshwa  kuhudhuria warsha ya kupokea mafunzo fursa inapopatikana, kwenda likizo na maslahi yao  kufanywa kipaumbele.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa