WAFANYIBIASHARA SITATUNGA WAHIMIZWA KUWEKA KAMERA ZA CCTV KWENYE MADUKA KUDHIBITI UHALIFU.

Chifu wa Kata ya Sitatunga katika Kaunti ya Trans Nzoia, Joseph Weyele amewawahimiza wafanyabiashara  kutundika kamera za CCTV katika majengo yao ili kuimarisha usalama na vilevile kuhifadhi data zinazoweza kutumika kama ushaidi utovu wa usalama unaposhuhudiwa.

Akilirejelea tukio la wizi ambalo Afisa wa polisi wa Akiba, NPR aliyeuliwa kwa kupigwa risasi  na  genge la majambazi ambalo vilevile  lilimjeruhi afisa wa polisi na mwananchi mmoja katika soko la Sibanga  kabla kutoweka na kitita cha pesa kisichojulikan, Wayele amesema oparesheni ya kulisaka genge hilo limeanzishwa.

Aidha ametumia fursa hiyo kuwarai wananchi kushirikiana na viongozi wa mpango wa nyumba kumi kuwaripoti watu wanaowashuku kuwa wahalifu ili kuhojiwa na kuajibishwa.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa