ERIC OMONDI ATAKA WADHFA WA UBALOZI WA SEKTA YA UTALII NCHINI.

You are currently viewing ERIC OMONDI ATAKA WADHFA WA UBALOZI WA SEKTA YA UTALII NCHINI.
  • Post category:Burudani

Mchekeshaji wa humu nchini Eric Omondi ametia nia ya kutaka nafasi ya ubalozi wa sekta ya utalii nchini.

Wadhfa huo ambao juzi kati ulipewa mwanamitindo wa Uingereza Naomi Campbell, utahusisha kutangaza  Kenya kama kituo cha utalii kimataifa.

Omondi ameshare ujumbe kwenye ukurasa wake wa Instagram akielezea ni kwanini anafaa apewe kazi hiyo, huku akitoa mfano wa matukio mbali mbali ambayo ameyatangazia Kenya kimataifa bila malipo yoyote.

Aidha ameenda mbali zaidi na kumpendekeza mshindi wa tuzo ya Oscar, Lupita Nyong’o kuteuliwa kama naibu wake kwenye wadhfa wa  ubalozi wa utalii.

Hata hivyo Eric Omondi amedokeza kwamba ana mpango wa kukutana na Waziri wa Utalii nchini Najib Balala kujadiliana kuhusu suala hilo.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa