DIAMOND PLATINUMZ AMTAJA Q CHIEF KAMA MSANII WAKE WA MUDA WOTE.

You are currently viewing DIAMOND PLATINUMZ AMTAJA Q CHIEF KAMA MSANII WAKE WA MUDA WOTE.
  • Post category:Burudani

Pamoja na kutokuwepo kwa maelewano mazuri kati yao Staa wa mzuiki wa Bongo Fleva na Mkurugenzi wa WCB na Wasafi Media Diamond Platnumz ameweka wazi kuwa Q Chief ndiye msanii wake bora wa muda wote na wimbo wa Nitampata Wapi ndio wimbo wake bora wa muda wote

Diamond amepost video kupitia Insta Story yake kwenye mtandao wa Instagram akiuangalia na kuimba wimbo huo kisha kuandika “Wimbo wangu bora wa muda wote, msanii wangu bora wa muda wote haijalishi kimetokea nini”

Wawili hao hivi karibuni walikuwa na vuta nikuvute baada ya Q Chief kulalamika picha yake na jina lake kutumika kwenye tangazo la wasanii watakaotumbuiza kwenye Tamasha la tumewasha Tour Jijini Dar es Salaam huku akiwa hajafanya mazungumzo yeyote ya kibiashara na waandaaji wa Tamasha hilo.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa