KALIFAH AGANAGA “BOB WINE ALICHANGIA KUSHINDWA KWA CHAMELEONE KWENYE UCHAGUZI WA UMEYA WA JIJI LA KAMPALA.”

You are currently viewing KALIFAH AGANAGA “BOB WINE ALICHANGIA KUSHINDWA KWA CHAMELEONE KWENYE UCHAGUZI WA UMEYA WA JIJI LA KAMPALA.”
  • Post category:Burudani

Msanii wa muziki kutoka Uganda Kalifah Aganaga anazidi kumtolea uvivu kinara wa chama ha kisiasa cha NUP, Bobi Wine.

Akipiga stori na runinga moja nchini Uganda Kalifah Aganaga amesisitiza kuwa Bobi Wine ana ubinafsi mwingi na hajawahi watakia mazuri wanamuziki wengine.

Mkali huyo wa ngoma ya “Kiboko” ameenda mbali zaidi na kudai kuwa kushindwa kwa Chameleone kwenye kinyang’anyiro cha umeya wa jiji la Kampala kulichangiwa na Bobi Wine ambaye alimnyima bosi huyo wa lebo ya muziki ya Leone tiketi ya chama cha NUP.

Ikumbukwe Jose Chameleone alishindwa vibaya na Erias Lukwago aliyepo madarakani kwa sasa kwenye uchaguzi wa umeya wa jiji la Kampala ambao ulikuwa na ushindani mkali.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa