Staa wa muziki wa Hip Hop nchini Tanzania, Rapa Country Boy kutoka lebo ya Konde Gang ya Harmonize amefunguka ukimya wa wasanii Killy na Chidi ambao tangu wamehamia kwenye lebo hiyo wakitokea Kings Music ya Alikiba wamekuwa kimya kwenye kuachia kazi.
Akizungumzia suala hilo ambalo mashabiki wengi wamekuwa wakihoji juu ya ukimya wao, Country Boy amesema, “Ukimya wa Killy na Chidi umesababishwa na ubize wa kutengeneza Album ambayo kila mmoja ataachia hivi karibuni.
Aidha, tangu alivyosainiwa Konde Gang rapa Country Boy tayari ameshaachia EP moja iitwayo “The Father EP” na kwa sasa anatamba na ngoma yake mpya iitwayo ‘Baby’.