CIND SANYU-“MUZIKI WANGU NI MKUBWA KULIKO TUZO ZA MTV MAMA.”

You are currently viewing CIND SANYU-“MUZIKI WANGU NI MKUBWA KULIKO TUZO ZA MTV MAMA.”
  • Post category:Burudani

Staa wa muziki nchini Uganda  Cindy Sanyu amesema  kwamba hajutii kukosa kwenye orodha ya wasanii walioteuliwa kuwania tuzo za  MTV MAMA Awards.

Kulinga na Cindy Sanyu  kutotajwa kwake kwenye tuzo hizo haitabadilisha chochote kwenye maisha yake ikizingatiwa kuwa tayari ana mafanikio makubwa kwenye muziki wake.

Kauli ya cindy inakuja mara baada ya wadau wa muziki nchini Uganda kudai kwamba msanii huyo alikasirika baada ya jina lake kukosa kwenye orodha ya wasanii waliotajwa kuwania tuzo za MTV MAMA.

Ikumbukwe Cindy alikuwa amependekeza tuzo za  MTV MAMA ziahirishwe  kwa kigezo kuwa Waganda wana masuala mengi neambayo yamewaathiri kutokana na janga la Corona huku akipinga hatua ya waandaji wa tuzo hizo kumleta DJ Khaled kutoka nchini Marekani awe mshereheshaji wa tuzo hizo.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa