NADIA MUKAMI AIBUA HISIA MSETO MIONGONI MASHABIKI BAADA YA KUJITANGAZA KUWA MWANDISHI BORA WA NYIMBO NCHINI.

You are currently viewing NADIA MUKAMI AIBUA HISIA MSETO MIONGONI MASHABIKI BAADA YA KUJITANGAZA KUWA MWANDISHI BORA WA NYIMBO NCHINI.
  • Post category:Burudani

Nyota wa muziki nchini Nadia Mukami ameibua mjadala mzito kwenye mtandao wa Twitter mara baada ya kudai kwamba yeye ndiye mwandishi bora wa nyimbo wa kizazi chake.

Kupitia misururu ya tweets kwenye ukurasa wake wa Twitter  mkali huyo wa Ngoma ya “Kolo” amependekeza kuwepo kwa tuzo za  mwandishi bora wa mwaka nchini huku akidai kwamba  pana haja ya wadau wa muziki nchini kuelekeza mawazo yote kwenye suala la uandishi wa nyimbo.

Haikushia hapo mrembo huyo alienda mbali zaidi na kusema kwamba amefurahia kuibua mjadala kuhusu uandishi wa nyimbo kwenye kiwanda cha muziki nchini kwani ni suala mtambuka ambalo linapaswa kuangaliwa kwa jicho la tatu.

Kufuatia kauli hiyo ya Nadia Mukami kuhusu suala la uandishi wa nyimbo imeibua hisia mseto miongoni mwa wakenya kwenye mtandao wa Twitter  ambapo baadhi wameonekana kuunga mkono madai ya msanii huyo huku wengine wakitofautiana nae wakidai kwamba wao sio mashabiki wa muziki wake.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa