Mwanamuziki kutoka nchini Uganda Chozen Blood hatimaye ameachia rasmi album yake mpya iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu na mashabiki zake.
Album hiyo ambayo ameipa jina la “Am Chozen” ina jumla ya ngoma 11 za moto huku, akiwa na ameshirikisha wasanii mbali mbali nchini uganda akiwemo John Blaq, na Fik Fameica.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Chozen Blood ambaye anafanya vizuri na wimbo wake wa “Sharp Shooter” amewashukuru maprodyuza waliosimamia mchakato wa kuitayarisha album hiyo na hatimaye kuitoa.
Album ya “Am Chozen” inapatikana ‘exclusive’ kupitia mitandao yote ya kukisikiliza na kuuza muziki duniani kama vile Boomplay, Spotify na Apple Music.