BEBE COOL ADAIWA KUWATAPELI WASANII KUTOKA JAMII YA KARAMOJA.

You are currently viewing BEBE COOL ADAIWA KUWATAPELI WASANII KUTOKA JAMII YA KARAMOJA.
  • Post category:Burudani

Wasanii kutoka jamii ya Karamoja nchini Uganda wameshtumu vikali staa wa muziki nchini humo Bebe Cool kwa madai ya kuwapa ahadi ya uongo.

Kwa mujibu Evy Trey mmoja wa wasanii kutoka Karamoja Bebe Cool aliwagiza watumie pesa zao kurekodi nyimbo za kampeini kwa ajili  Rais Yoweri Museveni na baadae watalipwa gharama zote walizozitumia kwenye suala la uandaaji wa nyimbo hizo lakini mpaka sasa hawajepokea pesa zozote.

Hata hivyo Juhudi za Jarida la Press Time nchini uganda kumtafuta bebe cool azungumzie suala hilo hazikuzaa matunda kwani simu zake zote zilikuwa zimezimwa.

Kauli ya wasanii hao inakuja siku chache baada ya msanii chipukizi nchini uganda aitwaye Zulunda kujitokeza na kumsuta vikali bebe cool kwa madai kwamba alikimbia na pesa zake kupitia wimbo wa mwongedde Akululu aliomuandikia msanii huyo kwa ajili ya kampeini za uchaguzi uliopita nchini Uganda. 

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa