MSANII PASCOL TOKODI AWACHANA WANAOMSHAMBULIA MITANDAONI MARA BAADA YA KUKUTANA NA RAIS UHURU KENYATTA.

You are currently viewing MSANII PASCOL TOKODI AWACHANA WANAOMSHAMBULIA MITANDAONI MARA BAADA YA KUKUTANA NA RAIS UHURU KENYATTA.
  • Post category:Burudani

Msanii wa muziki nchini Pascal Tokodi ambaye pia ni muigizaji amewatolea uvivu wanaomkashifu baada ya kuwambia Rais Uhuru Kenyatta atazame kipindi chake cha Selina kwenye moja ya  video inayosambaa mitandaoni.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Tokodi amesema hajutii kumwambia Rais afutilie kipindi cha Selina ambacho kinaruka kupitia runinga Maisha Magic East huku akisema hatotisha na maneno ya watu mitandaoni kwani alihamua kuzitumia sekunde 15 alizokutana na rais kenyatta kujitetea kuhusiana na shughuli yake ya uigizaji.

Kauli yake inakuja mara baada ya watu kumshambulia kwenye mitandao ya kijamii kwa kushindwa kumuuliza  Rais  Uhuru Kenyatta masuala muhimu ambayo kwa njia moja au nyingine yangemsaidia kimaisha.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa