BAHATI AFUNGUKA KUHUSU SUALA LA WATU KUMUITA “MTOTO WA DIANA”

You are currently viewing BAHATI AFUNGUKA KUHUSU SUALA LA WATU KUMUITA “MTOTO WA DIANA”
  • Post category:Burudani

Staa wa muziki nchini Kevin Bahati amefunguka kuhusu suala la watu kumuita mtoto wa Diana.

Kupitia ukurusa wake wa Instagram mkali huyo wa ngoma ya ‘Tomato” amesema haoni shida yeyote watu wakimuita mtoto wa diana kwani mke wake huyo anamuonyesha mapenzi aliyokosa kutoka kwa mamake mzazi ambaye alitangulia mbele za haki.

Haikuishia hapo bahati alienda mbali zaidi na kuweka wazi kwamba kipindi wanachumbiana na mkewe diana marua aliwahi kumuueleza kwamba  anatamani kumuona akimuonyesha mapenzi kama ya mamake mzazi.

Hata hivyo  baada ya kuona ujumbe huo mkewe Diana Marua alijibu kwa kusema kuwa hawezi kumpa msanii huyo mapenzi kama ya mamake mzazi bali atampa mapenzi kama mkewe.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa