Maaambukizi ya COVID19 Nchini humo yanatajwa kuwa makubwa kuliko ilivyoripotiwa awali kwa mujibu wa utafiti wa Kituo Cha Kuzuia na Kudhibiti Magonjwa Nigeria (NCDC).
Utafiti huo umefanyika Septemba na Oktoba 2020 na umebaini katika majimbo ya Lagos, Enugu na Nasarawa Mtu mmoja kati ya watano ana maambukizi ya Corona Virus.
Lagos inakadiriwa kuwa na watu milioni 4 wenye maambukizi tofauti na 54,000 ambao wameripotiwa. Mkuu wa NCDC amesema matokeo ya utafiti huo yamefanya juhudi za kutafuta chanjo kuwa muhimu zaidi