Mwakilishi wa Wodi mteule Kaunti ya Pokot Magharib Elijah Kasheusheu amelaani na kushutumu utovu wa usalama unaoendelea kushuhudiwa katika eneo la Kapedo.
Kwenye mahojiano ya kipekee na Northrift Radio, Kasheusheu amesema Serikali inafaa kuwakamata washukiwa waliotekeleza uovu huo mara moja ili sheria ifuate mkondo.
Kasheusheu aidha anapinga oparesheni ambayo Serikali imeanzisha eneo hilo akisema kuwa huenda Raia wasio na hatia wakaumia kufuatia maafisa wa Polisi kutumia nguvu kupita kiasi.
Nao wakaazi Kaunti ya Pokot Magharibi wakiongozwa na Musa Chepareraka, Paul Kamama. julius Merikit wamekashifu kitendo hicho na kuilaumu Serikali kwa kuanzisha oparesheni Kapedo badala ya kuwakamata washukiwa kwanza.
Kwa upande wake Stephen Kolimuk kiongozi wa amani Pokot Magharibi amehoji kuwa ni jukumu la Serikali kuhakikisha kuwa inawalinda wananchi wake ikizingatiwa kuwa mwananchi yeyote ana haki ya kuishi popote.