ZAIDI YA WATU ELFU 70 WAFANYIWA VIPIMO VYA CORONA TURKANA

Zaidi ya watu elfu 70 katika kaunti ya Turkana wamefanya vipimo vya Corona kama njia moja ya kudhibiti kuenea kwa virusi vya covid 19 kaunti hiyo.

Akiongea na meza yetu ya habari Afisa katika Wizara Afya kaunti ya Turkana Dakta Gilchrist Lokoel amesema  zoezi hilo lilifanywa  kwenye kaunti ndogo  zote kaunti hiyo ambapo watu 23,256 wamefanywa vipimo Turkana Kusini,Turkana ya Kati watu 35,884,Turkana Magharibi watu  5,779,Turkana Mashariki watu 2,750, Loima watu 1034 na Kibish watu 44.

Aidha amesema watu wote 72,401 ambao walifanyiwa vipimo  wamepatikana hawana maambukizi ugonjwa wa  corona ambao unasababishwa na virusi vya covid-19.

Hata hivyo amesema kuwa serikali ya kaunti inaendelea kuweka mikakati kuhakikisha janga la corona linadhibitiwa kwani wahuduma wa afya wametumwa kila kona ya kaunti hii kutoa elimu kwa umma dhidi ya corona.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa