WASANII CARDI B,TAYLOR SWIFT,HARRY STYLES NA WENGINE KIBAO KUTUMBUIZA KATIKA TUZO ZA 63 ZA GRAMMY 2021.

You are currently viewing WASANII CARDI B,TAYLOR SWIFT,HARRY STYLES NA WENGINE KIBAO KUTUMBUIZA KATIKA TUZO ZA 63 ZA GRAMMY 2021.
  • Post category:Burudani

Waandaaji wa Tuzo kubwa za muziki Duniani Grammy  wametangaza list ya wasanii watakaotumbuiza katika hafla ya utoaji Tuzo za 63 za Grammy mwaka  wa 2021.

Rapa Cardi B, Megan Thee Stallion na Lil Baby wametajwa kudondosha Burudani wakati wa hafla hiyo inayotarajiwa kufanyika Machi 14, mwaka 2021 huko Los Angeles, nchini Marekani.

Roddy Ricch ,Post Malone, Doja Cat, DaBaby, na Taylor Swift pia watatumbuiza wakati wa sherehe hiyo, ambayo itazingatia miongozo ya usalama wa COVID-19.

Wasanii wengine ni pamoja na Dua Lipa, BTS, Harry styles, Bad Bunny na Chris Martin.

Katika Tuzo za Grammy 2021 Beyoncé ndiye ameteuliwa katika Vipengele 9 akifuatiwa na Taylor Swift, Dua Lipa, na Roddy Ricch wakiwa na Vipengele sita kila mmoja.

Host wa Sherehe ya Tuzo hizo za kila mwaka atakuwa Trevor Noah kutoka Afrika kusini na, itaruka Mubashara kwenye runinga ya CBS  Machi 14, mwaka huu baada ya kuahirishwa Januari 31 kutokana na kuongezeka kwa visa vya COVID-19 huko Los Angeles.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa