WAWAKILISHI WADI TURKANA WATAKIWA KUPITISHA BBI

You are currently viewing WAWAKILISHI WADI TURKANA WATAKIWA KUPITISHA BBI

Wawakilishi wadi kaunti ya Turkana wametakiwa kupitisha ripoti ya BBI kwani  inapendekeza nyongeza ya ugavi wa fedha kwa serikali za kaunti ambayo italeta maendeleo mashinani.

Akizungumza kwenye mkutano wa BBI mjini Lodwar Waziri wa Mafuta na Madini John Munyes amesema kuongezwa kwa mgao wa fedha za kaunti kutoka asilimia 15 hadi 35 itachangia pakubwa kuendeleza miradi ya maendeleo kaunti hiyo.

Aidha Munyes ameongeza kuwa pendekezo la kubuniwa kwa hazina ya maendeleo ya wadi katika ripoti ya BBI itachangia katika utekelezwaji wa miradi ya maendeleo mashinani.

Sanjari na hilo ametoa wito kwa serikali ya kitaifa kutoa msaada wa chakula kwa wakaazi wa kaunti ya Turkana ambao anadai wameathirika na makali ya njaa.

Kuhusu suala la usalama mshirikishi wa BBI kaunti ya Turkana Beatrice Asukul ameitaka serikali ya kitaifa kupitia Wizara ya Usalama wa Ndani kuihimarisha usalama eneo la Kapedo hata baada ya operasheni kukamilika ili kuwaondolea wananchi hofu ya kushambulia tena na majangili.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa