WAWAKILISHI WADI TRANS NZOIA WAKANUSHWA KUPEWA RUSHWA KUUNGA MKONO BBI.

Wawakilishi wadi katika bunge la kaunti ya Trans-Nzoia wamepuuzilia mbali madai kwamba ruzuku ya shilingi milioni nne nukta tano ya magari kwa wabunge wa kaunti kote nchini imetumika kuwahonga ili kuunga mkono ripoti ya maridhiano BBI.

Kulingana na mwakilishi wadi mteule  katika bunge hilo Philip Nyongesa amesema kilichofanyika tu ni kubadilisha mikopo ya kununua magari kuwa ruzuku ambayo imekuwa katika makadirio ya kifedha ya mwaka iliyotangulia.

Kwa upande wake mwakilishi wa wadi yaSaboti David Kapoloman amewataka wabunge wa kitaifa kukoma kuingilia mabunge ya kaunti na badala yake waendelee kutekeleza majukumu yao.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa