WANASIASA WATAKIWA KUSITISHA SIASA KWENYE HAFLA ZA MAZISHI TRANS-NZOIA.

Wanasiasa wamehimizwa kusitisha cheche za matusi kwenye majukwaa ya mikutano ya hadhara na mazishini ili kupunguza joto la kisiasa ambalo linaendelea kupanda kila kuchao.

Akihutubu wakati wa mazishi kwenye eneo la Marambach Kitalale, Afisa Mkuu Mtendaji katika Wizara ya Maji, Mazingira na Maliasili katika kaunti ya Trans nzoia, John Meng’wa amesema Kenya inaweza kustawi kiuchumi na kimaendeleo iwapo viongozi wataendelea kuhubiri umoja na utangamano.

Meng’wa amewashauri viongozi kusitisha siasa mazishini na badala yake kuifariji na  kuipa familia iliyofiwa muda mwafaka wa kuomboleza.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa