WAKULIMA VIHIGA KUFAIDI NA NGOMBE 47 KUTOKA KWA SERIKALI YA KAUNTI.

You are currently viewing WAKULIMA VIHIGA KUFAIDI NA NGOMBE 47 KUTOKA KWA SERIKALI YA KAUNTI.
  • Post category:Biashara

Wafugaji wa ngombe wa maziwa katika kaunti ya Vihiga wamepigwa jeki baada ya kaunti hiyo kutoa ng’ombe 47 kwa makundi ya wakulima mbalimbali ili kuimarisha uzalishaji wa kiwango cha maziwa.

Gavana wa kaunti hiyo Wilber Otichilo ametoa changamoto kwa wakulima kujisatiti ili kuhakikisha uzalishaji wa maziwa unaongezeka.

Katika kipindi cha miaka mitatu kaunti hiyo imepeana zaidi ya ngombe 250 wa maziwa bila malipo kwa makundi ya wakulima.

Hata hivyo wakulima wanasema kwamba hatua hiyo itawasaidia pakubwa kuwapa ajira.

Kadhalika gavana Otichilo amewashauri wakulima kuwasiliana na kitengo cha kilimo kaunti hiyo iwapo watahitaji ushauri kuhusu kilimo.

Kulingana na gavana Otichilo, anapanga kujenga kiwanda cha maziwa ili kuinua kipato cha wakulima wanaopatikana eneo hilo,

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa