WAKAAZI WA SIYOI ENEO BUNGE LA KAPENGURIA WAFAIDI NA KONDOO KUTOKA KWA SERIKALI YA KAUNTI

You are currently viewing WAKAAZI WA SIYOI ENEO BUNGE LA KAPENGURIA WAFAIDI NA KONDOO KUTOKA KWA SERIKALI YA KAUNTI
zaidi ya kondoo 100 wakabidhiwa wenyeji siyoi

Serikali ya kaunti ya Pokot Magharibi kwa ushirikiano na shirika la Kenya smart climate limetoa kondoo zaidi ya mia moja kwa wakaazi wa Siyoi.

Waziri wa kilimo kaunti hiyo Godfrey Lipale anasema kondoo hao wamefanyiwa utafiti na wana uwezo wa kuzaana mara mbili kwa mwaka kando na kuwapa wananchi maziwa yenye madini akisema wakulima watafaidi pakubwa.

Aidha anasema wakulima ambao wamekaguliwa na kuidhinishwa na Wizara ya kilimo ndio watakaofaidi na kondoo hao.

Alex Toilem

Mwandishi, mhariri na msomaji wa habari Northrift Radio 104.9/104.5FM kapenguria.