WAKAAZI WA NAREWA KAUNTI NDOGO YA TURKANA YA KATI WAANDAMANA KULALAMIKIA BOMBA LA MAJI AMBALO LIMEWASABABISHIA HASARA

Wakaazi wa Narewa wadi ya Kanamker kaunti ndogo ya Turkana ya Kati wameandamana kulalamikia kampuni ya ujenzi ya China Railway 5 kwa ujenzi mbaya wa bomba la kupitisha maji taka ambalo huenda likaathiri shughuli zao.

Wakaazi hao wakiongozwa na mzee Calis Emanikor ambaye ni mzee wa kijiji cha Narewa,kilichoko wadi ya Kanakemer wamesema  hawataruhusu kampuni hiyo iendelee na shughuli ya ujenzi wa barabara katika eneo hilo hadi pale serikali ya kaunti itakaposikiliza lalama zao. 

Aidha wamesema eneo hilo linakumbwa na uhaba mkubwa wa  maji jambo ambalo wamesema limeathiri suala nzima la kupambana na janga la corona.

Hata hivyo mtawala wa wadi ya Kanamkemer Shaban Etabo amewataka wakaazi hao wawe na subira wakati huu uongozi wa wadi hiyo unashughulikia matakwa yao.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa