WAHU AWATOLEA UVIVU BAADHI YA WATU WANAODAI AMERUDI TENA KWENYE MUZIKI WA KIDUNIA.

You are currently viewing WAHU AWATOLEA UVIVU BAADHI YA WATU WANAODAI AMERUDI TENA KWENYE MUZIKI WA KIDUNIA.
  • Post category:Burudani

Mwanamuziki wa nyimbo za injili nchini Wahu amejibu juu ya madai yaliyoibuliwa na baadhi ya wakenya kwenye mitandao ya kijamii kuwa amerudi kwenye muziki wa kidunia mara baada ya kuuachia wimbo wa mapenzi.

Kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa instagram Wahu amefunguka na kusema kwamba hajutii kutunga wimbo wa mapenzi uitwao “This Love Ya Wahu” kwani kufanya hivyo sio dhambi.

Aidha amesema katika maisha suala la mapenzi limetawala, hivyo kitendo chake cha kutunga wimbo wa mapenzi hakiendi kinyume na imani yake huku akisisitiza kwamba hajeacha kumtumkia Mungu.

Ikumbukwe wahu alitangaza kuacha muziki wa kidunia mwaka wa 2017 na kuhamia kwenye muziki wa injili mara baada ya kuachia wimbo wake uitwao “Sifa.”

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa