WACHOMA MKAA KACHELIBA,POKOT MAGHARIBI WAONYWA

You are currently viewing WACHOMA MKAA KACHELIBA,POKOT MAGHARIBI WAONYWA

Wakazi wa eneo Bunge la Kacheliba wametahadharishwa dhidi ya kuharibu misitu kwa kukata miti na kuchoma makaa na wengine kuiuza kwa matapeli wanaodaiwa kusafirisha miti hiyo kutoka eneo hilo na kuivusha nchini jirani ya Uganda bila idhini.

Akizungumza na kituo hiki kwa njia ya simu, Afisa wa misitu katika eneo la Kacheliba Damiano Morlem, amesema miti ya kiasili iko kwenye hatari ya kumalizika iwapo wananchi hawataitunza kikamilifu.

Damiano amesema kumekuwapo na changamoto za kuwakabili wahalifu hao hasa wanaotoka nchini uganda, japo amewaonya kwamba sheria itachukua mkondo wake kwa yeyote atayepatikana akikaidi amri hiyo.

Kwa upande wake Meshack Lomang’ura ambaye pia ni afisa katika idara hiyo, amewasihi wakazi wa kaunti ya Pokot Magharibi kuchukua jukumu la kutunza misitu bila kushurutishwa.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa