VIONGOZI TURKANA WATAKA USALAMA UHIMARISHWE MPAKANI MWA KENYA NA SUDAN KUSINI.

Viongozi kutoka katika kaunti ya Turkana wameonyesha wasiwasi wao kutokana na ongezeko la visa vya ukosefu wa usalama katika baadhi ya sehemu za kaunti hiyo hasa zile zinazopakana na nchi ya sudan kusini na Ethiopia.

Akizungumza mjini lodwar Mbunge wa Turkana Magharibi Daniel Epuyo amesema wakaazi wanaoishi mpaka mwa nchini hizo wamepoteza maisha yao huku akitaka  serikali kuwatuma maafisa zaidi ya usalama kushika doria katika eneo hilo kwani wenyeji wanaisha na hofu ya kushambuliwa na magaidi.

Kwa upande wake mbunge wa Loima Jeremiah Lomurkai ameitaka serikali kuu kuendesha operasheni inayoendelea mpakani mwa kaunti ya Turkana na Baringo bila upendeleo hadi pale majangili wanaotatiza amani eneo hilo watakaposalimia amri.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa