VIONGOZI NCHINI WATAKIWA KUACHA SIASA ZISIZO NA TIJA.

You are currently viewing VIONGOZI NCHINI WATAKIWA KUACHA SIASA ZISIZO NA TIJA.

Seneta wa Siaya ambaye pia ni kiongozi wa wachache katika bunge la seneti James Orengo amewataka wafanyikazi wa serikali kukoma kutumia muda wao mwingi katika maswala ya siasa na badala yake kuwatumikia wananchi

Orengo amewataka viongozi wote nchini kushirikiana na rais Uhuru Kenyata kuhakikisha mshikamano wa kitaifa kupitia ripoti ya upatanishi BBI.

Aidha ameongeza kuwa muda wa  kufanya siasa haujafika na itakuwa vema iwapo ajenda za maendeleo zitapewa kipau mbele

Ni kauli ambayo imeungwa mkono na gavana wa Machakos dakta Alfred Mutua akisema hatua ya viongozi wa kisiasa kurushiana cheche za maneno hadharani inatishia umoja wa kitaifa.

Kulingana na Mutua hakuna maendeleo ambayo inaweza kuafikiwa katika nchini yoyote ikiwa siasa ndo lugha ya pekee wanayojua wakenya kutoka kwa viongozi.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa