VIJANA KAUNTI YA POKOT MAGHARIBI WAHIMIZWA KUWANIA VITI MBALI MBALI KATIKA UCHAGUZI MKUU UJAO

Vijana kaunti ya Pokot Magharibi wameshauriwa kujihusisha na maswala ya siasa kwa kuwania viti mbali mbali ili nao waweze kuwa ndani ya serikali.

Kulingana na Katelem Josephat, kwa kipindi kirefu vijana wametumika vibaya na sasa ni zamu yao kujituma.

Aidha Katelem ameskitikia hatua ya baadhi ya wanasiasa kuwashinikiza Wakaazi Pokot Magharibi kuisoma ripoti ya mapendekezo ya BBI wakati wananchi hawajapata nakala ya ripoti hiyo.

Anasema itakuwa vigumu kwa mwananchi kuipigia kura ripoti asiyoielewa.

Alex Toilem

Mwandishi, mhariri na msomaji wa habari Northrift Radio 104.9/104.5FM kapenguria.