Mkali wa muziki nchini Victori Kimani amedaiwa kuiba wimbo unaofanya vizuri kwa sasa unaokwenda kwa jina la ‘Africana’ aliyomshirikisha msanii Silverstone Barz.
Kikundi cha muziki wa hip hop nchini ‘SDP’ limedai kwamba Victoria Kimani amekuwa na tabia ya kuiba nyimbo zao lakini wamekuwa kimya kwa muda mrefu ila sasa wameamua kuvunja ukimya wao.
Kauli hiyo iliibua hisia mseto miongoni mwa mashabiki wa kundi la “SDP” ambao waligundua kuwa mdundo uliotumika kwenye wimbo wa Victoria Kimani uitwao “Africana” unafanana na wimbo wao uiitwao “Vengai” na hivyo kudhibitisha madai yaliyoibuliwa na member wa kundi hilo Sean Mpreezy.