“SIFANYI MUZIKI KWA AJILI YA TUZO”-ASEMA OCTOPIZZO

You are currently viewing “SIFANYI MUZIKI KWA AJILI YA TUZO”-ASEMA OCTOPIZZO
  • Post category:Burudani

Mwanamuziki wa hiphop nchini Octopizzo amefunguka na kusema kuwa yeye hafanyi muziki ili kupata au kushinda tuzo.

Kupitia mtandao wa kijamii wa Twitter Octopizzo amewataka mashabiki wa muziki wake watambue kuwa yeye hafanyi muziki ili kupata tuzo bali anafanya muziki kutoa burudani, pamoja na kumuingizia kipato, hivyo ndio maana siku zote huwa anajiita mwanamuziki mfanyabiashara.

Kauli hiyo ya Octopizzo imekuja mara baada ya wadau wa muziki nchini kumshinikiza kufanya collabo na wasanii wa kimataifa  ili aweze kuteuliwa kushiriki kwenye tuzo kubwa za muziki duniani za BET kwa lengo la kuupeleka muziki wa Kenya kimataifa.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa