SEKTA YA KIVIWANDA INATARAJIWA KUONA MWANGA WA JUA GATUZI LA POKOT MAGHARIBI

You are currently viewing SEKTA YA KIVIWANDA INATARAJIWA KUONA MWANGA WA JUA GATUZI LA POKOT MAGHARIBI
Gavana Lonyangapuo aweka jiwe la msingi

Serikali ya kaunti ya Pokot magharibi imeangazia zaidi kuweka dhamana katika bidhaa za maziwa kwa kuanzisha kiwanda cha maziwa katika eneo la Kabichbich Pokot kusini.

Akizungumza baada ya kuweka jiwe la msingi katika eneo la ujenzi wa kiwanda hicho gavana John Lonyang’apuo amelezea faidi nyingi ambazo wafugaji wa ng’ombe wa maziwa watapata kutokana na kilimo hicho.

Lonyang’apuo ametoa hakikisho kwa wakulima kwamba kiwanda hicho kitafungua mianya ya vijana wengi kupata ajira sawa na kuongezeka kwa bei ya maziwa.

Ni kauli ambayo imeungwa mkono na waziri wa kilimo Godfrey lipale ambaye anasema serikali inalenga kuhakikisha visa vya ufugaji wa kuhamahama inapunguzwa na kutoa nafasi kwa wakulima kukumbatia kilimo cha ng’ombe wa maziwa

Ameongeza kuwa malengo ya uongozi wa Gavana Lonyang’apuo inaenda sambamba na ajenda za utawala wa rais Uhuru Kenyatta kuhusu ustawishaji wa viwanda na kuinua viwango vya uzalishaji.

Alex Toilem

Mwandishi, mhariri na msomaji wa habari Northrift Radio 104.9/104.5FM kapenguria.