SAUTI SOL KUZINDUA BIDHAA ZA EARBUD KWA USHIRIKIANO NA KAMPUNI YA PACE AFRICA.

You are currently viewing SAUTI SOL KUZINDUA BIDHAA ZA EARBUD KWA USHIRIKIANO NA KAMPUNI YA PACE AFRICA.
  • Post category:Burudani

Kundi la muziki nchini Sauti Sol limesaini mkataba na kampuni ya Pace Africa kutengeneza spika ndogo za masikioni (EarBuds) ziitwazo PaceSol.

Sauti sol wametumia ukurasa wao wa Instagram kuwataharifu mashabiki wao kuhusu mpango wao wa kuja na bidhaa mpya ambazo zitawatambulisha kama kundi.

Kulingana na wakali hao wa ngoma ya Suzzana, PaceSol itakuwa ni bidhaa yao ya kwanza kwa ushirikiano  na kampuni ya Pace Africa wakiwa na mpango pia wa kuzindua bidhaa nyingine za teknolojia kwenye ukanda huu wa Afrika Mashariki.

Hata hivyo wamesema bidhaa za PaceSol zinalenga kuwahimiza wafrika kuwa wabunifu kwenye masuala ya ujarisilimali huku wakifurahia muziki wao.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa