Msanii wa nyimbo za Injili nchini Ringtone Apoko amekosoa hatua ya Daddy Owen kusonga mbele na maisha yake hata kabla hajemaliza mchakato wa kutalikiana na mkewe Faridah Wambui.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram Ringtone ameweka wazi kuwa Daddy Owen ana mpango kufunga ndoa nyingine hivi karibuni.
Hii ni baada ya kushare picha ya daddy owen akiwa na mwanamke mmoja asiyejulikana na kudai kwamba msanii huyo ana mpango wa kumuoa mwanamke huyo.
Hata hivyo Hitamker huyo wa ngoma ya Omba amemtaka DJ Mo na Mkewe Size wamtafutie daddy owen mke.