RAPA MEEK MILL NA TEKASHI 69 WARUSHIANA MAKONDE HUKO ATLANTA NCHINI MAREKANI.

You are currently viewing RAPA MEEK MILL NA TEKASHI 69 WARUSHIANA MAKONDE HUKO ATLANTA NCHINI MAREKANI.
  • Post category:Burudani

Mastaa wa muziki wa Rap kutoka Nchini Marekani Meek Mill na Tekashi 69 karibu warushiane makonde baada kuingia kwenye mzozo mkali nje ya klabu moja  huko Atlanta, nchini Marekani.

Rappers hao walikuwa kwenye sherehe katika Night club moja huko Atlanta kabla ya kukutana kwenye eneo la Maegesho ya Magari, ambapo wameonekana katika video wakipiga kelele na kutukanana wakati wakizuiwa na Walinzi wao.

Wawili hao wali-share clip za tukio hilo katika Mitandao yao ya kijamii na kila mmoja akijaribu kuelezea tukio hilo kwa upande wake.

Ikumbukwe Meek Mill na Tekashi 69 wamekuwa katika bifu kwa miezi kadhaa sasa baada ya Meek mill kumuita tekashi  ‘Panya’ katika chapisho lake la mwezi mei mwaka wa 2020 katika mtandao wa twitter.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa