RAPA EAZI MONEY AMSUTA JAH CURE KWA KUMTISHIA MAISHA BAADA YA KUSHINDWA KUFANYA NAE COLLABO.

You are currently viewing RAPA EAZI MONEY AMSUTA JAH CURE KWA KUMTISHIA MAISHA BAADA YA KUSHINDWA KUFANYA NAE COLLABO.
  • Post category:Burudani

Rapa  Eazi Money kutoka nchini Jamaica amemsuta vikali msanii  nguli wa Reggae nchini humo  Jah Cure kwa hatua ya kushindwa kumaliza mashairi ya collabo yao aliyolipwa miaka minne iliyopita.

Kwa mujibu wa Eazi Money ambaye hapa kati alishare baadhi ya jumbe za vitisho kutoka kwa Jah Cure mitandaoni, hajefurahishwa na jinsi msanii huyo wa reggae alivyomtishia maisha, hivyo amewataka wadau wa muziki nchini Jamaica wamsaidia ili Jah Cure amlipe pesa zake kama suala la  collabo limeshindikana.

Hata hiyo Eazi Money amewashukuru mashabiki wake na wanablogu kwa kueneza chapisho lake na kuwafanya watu wafahamu kile Jah Cure amemtendea huku akitawataka wakae mkao wa kula kwa EP yake iitwayo “Reggae Vibe & Summer Nights” ambayo itaachia rasmi tarehe 28 mwezi huu wa Februari.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa