PROF. JOHN LONYANG’APUO “ELIMU NDIO NJIA YA KUMALIZA UKEKETAJI POKOT MAGHARIBI”

You are currently viewing PROF. JOHN LONYANG’APUO “ELIMU NDIO NJIA YA KUMALIZA UKEKETAJI POKOT MAGHARIBI”

Elimu ndio njia ya pekee itakayopelekea kumalizwa kwa visa vya ukeketaji miongoni jamii zinazoendeleza tamaduni hiyo ambayo imepitwa na wakati

Akizungumza katika maadhimisho ya siku ya kupambana na ukeketaji katika eneo la Alale Pokot Kaskazini gavana John Lonyangapuo anasema changamoto kuu ya kubali tamaduni hiyo ni ukosefu wa elimu miongoni mwa wanajamii ambao wamekuwa wakidhamini mila na itikadi bila kufahamu umuhimu wa elimu katika maisha ya baadaye

Lonyangapuo amekariri kujitolea kwa serikali yake kufanikisha juhudi za kuondoa ujinga na umaskini kupitia manifesto yake ambayo ni elimu usawa na kuimraisha uchumi ili kuafikia malengo ya kubadilisha taswira ya watu kuhusu kaunti ya Pokot Magharibi.

Kwa upande wake mkewe Mary Lonyangapuo ameelezea haja ya juhudi za pamoja miongoni mwa wanajamii ili kumaliza ukeketaji na kutimiza malengo ya serikali kumaliza utamaduni huwo kufikia mwaka wa 2022.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa