OTILE BROWN ATOA YA MOYONI KUHUSU SHINIKIZO WASANII WA KENYA WANAPATA KUTOKA KWA MASHABIKI.

You are currently viewing OTILE BROWN ATOA YA MOYONI KUHUSU SHINIKIZO WASANII WA KENYA WANAPATA KUTOKA KWA MASHABIKI.
  • Post category:Burudani

Nyota wa muziki nchini Otile Brown amewataka wasanii nchini kutokubali kupewa shinikizo na watu kwenye mitandao ya kijamii kwa kuwalinganishwa na wasanii waliowazidi kimuziki kutoka mataifa mengine.

Kupitia post ndefu aliyoichapisha kwenye ukurasa wake wa Instagram na kisha akaifuta Otile Brown amesema amechoshwa na kasumba ya watu kwenye mitandao kuwashindisha wasanii wa Kenya na  wasanii wengine wenye mafanikio makubwa kimuziki ikizingatiwa kuwa wasanii wengi nchini hawana watu wa kuwafadhili na kusimamia kazi zao.

Mkali huyo wa ngoma ya Dusuma amewataka wakenya kutowapa wasanii shinikizo zisozo kuwa na msingi kwani wengi wao wanajituma kwenye suala la kutoa muziki mzuri na kuupeleka muziki wa Kenya kimataifa.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa