NVIIRI THE STORYTELLER AACHIA “KITENGE EP” YENYE NGOMA 6

You are currently viewing NVIIRI THE STORYTELLER AACHIA “KITENGE EP” YENYE NGOMA 6
  • Post category:Burudani

Suala la kuachia EP, kwa sasa kwenye kiwanda cha muziki nchini, limekuwa likizidi kushamiri na kila msanii amekuwa akionyesha uwezo wake katika kazi zake. 

Sasa Msanii  Nviiri the Story teller kutoka Sol generatiom ameachia Ep yake mpya iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu na mashabiki zake.

Ep hiyo inayokwenda kwa jina la “Kitenge” imebeba ngoma sita za moto huku akiwa amewashirikisha wasanii kama Sanaipei Tande, Khalighraph Jones na Sauti Sol.

Hata hivyo Kitenge EP iliyotoka chini ya lebo ya muziki ya Sol Generation inayomilikiwa na Sauti Sol inapatikana exclusive kupitia digital platforms zote za kupakua na kusikiliza muziki duniani.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa