NANOK AKUTANA NA BALOZI WA UHALONZI NCHINI MAARTEN BROUWER

You are currently viewing NANOK AKUTANA NA BALOZI WA UHALONZI NCHINI MAARTEN BROUWER

Serikali ya kaunti ya Turkana imetia sahihi mkataba wa maelewano na ubalozi wa uholanzi nchini kuhimarisha ushiriki wa sekta ya kibinafsi  katika kuwekeza kwenye ukuaji wa sekta ya umma ili kuafikia malengo endelevu.

Akizungumza mjini Lodwar kwenye mkao na balozi wa uholanzi nchini gavana wa kaunti ya turkana Josphat Nanok  amesema mkao huo umepelekea kuzinduliwa kwa mpango wa prospects ambao unalenga kupiga jeki misaada ya kibinadamu na maendeleo kaunti hiyo hasa kwenye sekta ya elimu na nyanja zingine za kimaendeleo.

Nanok amesema serikali ya kaunti ya turkana ipo tayari kushirikiana na wadau mbali mbali wa maendeleo kufanikisha utekelezwaji mpango huo unaonuia kuwafaidi wakaazi wa kaunti hiyo.

Kwa upande wake Balozi wa Uholanzi  Maarten Brouwer ameeleza kuwa serikali ya uholanzi iko tayari kushirikiana na kaunti ya turkana katika kupambana na mabadiliko ya Tabia nchi na kuhakikisha utekelezwaji wa mpango wa maendeleo na kiuchumi wa kalobeyei unawafaidi wakimbizi na wakaazi kaunti hiyo kupitia mpango wa prospects.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa