MWANAMUZIKI CHRISTIAN WA KUNDI LA LONGOMBAS AFARIKI DUNIA

You are currently viewing MWANAMUZIKI CHRISTIAN WA KUNDI LA LONGOMBAS AFARIKI DUNIA
  • Post category:Burudani

Msanii wa Kundi maarufu la ‘Longombas’ kutoka Kenya Christian Longomba amefariki dunia, imeripotiwa kuwa umauti umemkuta katika Hospitali huko Los Angeles nchini Marekani akipatiwa matibabu.

Chanzo cha kifo chake kinatajwa kuwa ni ugonjwa wa uvimbe kwenye ubongo wake ‘brain tumor’ ambao amekuwa akipambana nao kwa muda wa miaka mitano sasa.

Mwezi Mei mwaka wa 2015, Christian aligundulika kuwa na uvimbe kwenye ubongo na alifanyiwa upasuaji kuuondoa. Upasuaji huo ulienda vyema lakini ilibidi apasuliwe tena mara baada ya madaktari kubaini kuganda kwa damu kwenye ubongo.

Kifo cha Christian kimethibitishwa na kaka’ke ambaye pia ni mwanamuziki mwenza Lovi Longomba. “Nakupenda Kaka yangu, Partner wangu na Rafiki yangu lakini Yesu amekupenda zaidi, uwe na furaha mbinguni” – ameandika Lovy.

Wawili hao ambao ni wapwa wa mwanamuziki Awilo Longomba walianza Muziki wakiwa nchini Kenya miaka ya 2000. Kundi la Longombas lilitamba na nyimbo kama vuta pumzi, shika more na dondosa.

Baadaye walihamia Marekani ambapo waliachana na muziki wa dunia na kuwa wahubiri wa injili.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa