MUUNGANO WA WALEMAVU TRANS NZOIA WASHANGAZWA NA IDADI YA JUU YA WAHUDUMU WA BODABODA WANAOLEMAA WAKIWA KAZINI.

Kundi la watu wenye ulemavu katika Kaunti ya Trans Nzoia limeelezea wasiwasi wake kwa kuongezeka kwa idadi ya watu wanaopata ulemavu wengi wao wakiwa wanabodaboda. 

Mwenyekiti wa Vijana wa Watu Wenye Ulemavu,  Ojiambo  Opis amesema wengine wa waendeshaji pikipiki wanaohusika kwenye ajali wameishia kukatwa miguu na baadhi yao kuwekewa vyuma kurejelea hali yao ya kawaida.

Kufuatia hilo Opis amesema wameanzisha kampeini ya kuhamasisha wanabodaboda kuhusu umuhimu ya kuzingatia sheria za trafiki, kuacha kutumia vileo wakiwa kazini na kuwaondoa watoto katika sekta hiyo.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa