MTU MMOJA AFARIKI HUKU MWINGINE AKIJERUHIWA VIBAYA KWENYE AJALI TURKANA.

You are currently viewing MTU MMOJA AFARIKI HUKU MWINGINE AKIJERUHIWA VIBAYA KWENYE AJALI TURKANA.

Mtu mmoja ameaga dunia huku mwingine akijeruhiwa vibaya baada ya gari walilokuwa wakisafiria kuhusika katika ajali ya barabarani, Kaunti ya Turkana.

Akithibitisha tukio hilo Afisa wa polisi Kaunti Ndogo ya Turkana ya kati Canningham Suiyenga amesema ajali hiyo imetokea baada ya gari lilokuwa likitoka Lodwar likielekea Kakuma kupoteza mweelekeo na kubiringika mara kadhaa, gurudumu lake lilipopasuka likiwa safarini.

Suiyenga amewasihi madereva kuwa waangalifu na kuzingatia sheria za barabarani ili kupunguza uwezekano wa ajali kutokea.

Hata hivyo aliyejeruhiwa kwenye ajali hiyo kwa sasa anaendelea kupokea matibabu katika hospitali ya misheni ya Kakuma huku mwili wa aliyeaga dunia ukihifadhiwa katika  ya hospitali ya Rufaa ya Lodwar.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa