MTIHANI WA KITAIFA KWA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI KUANZA MACHI- ASEMA MAGOHA.

You are currently viewing MTIHANI WA KITAIFA KWA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI KUANZA MACHI- ASEMA MAGOHA.

Sasa ni rasmi kwamba watahiniwa wa darasa la 8 na kidato cha nne wataanza mtihani wao wa kitaifa katika kipindi cha wiki 8 zijazo.

Waziri wa Elimu Prof. George Magoha amesema kuwa wanafunzi wa darasa la nane wataanza mtihani wao tarehe 19 mwezi Machi huku wale wa kidato cha nne wakianza tarehe 25 mwezi Machi akisema akiwataka watahiniwa kujiepusha na visa vya utovu wa nidhamu na kuweka juhudi zao kwa masomo.

Aidha Magoha amesema huenda serikali ikalazimika kurejesha adhabu ya viboko kufuatia kukithiri kwa visa vya utovu wa nidhamu miongoni mwa wanafunzi.

Hata hivyo amedai visa vinavyoshuhudiwa kwa sasa nchini hasa uteketezaji wa shule na uharibifu wa mali vinaweza kuwa vimechangiwa na hatua ya kutowaadhibu wanafunzi.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa