WEASEL MANIZO AWASHAURI WASANII WACHANGA WALIOFANYA VIZURI MWAKA 2020 NCHINI UGANDA NAMNA YA KUDUMU KWENYE MUZIKI BILA KUCHUJA.

You are currently viewing WEASEL MANIZO AWASHAURI WASANII WACHANGA WALIOFANYA VIZURI MWAKA 2020 NCHINI UGANDA NAMNA YA KUDUMU KWENYE MUZIKI BILA KUCHUJA.
  • Post category:Burudani

Msanii wa muziki wa Dancehall kutoka Weasel Manizo amewashauri wasanii wapya, Eezy wa ngoma ya Tumbiza Sound na Mudra, hitmaker wa Muyayayu kutopumzika iwapo wanataka kubaki kwenye kiwanda cha muziki nchini humo kwa muda mrefu.

Kwenye moja ya interview, Weasel amesema wasanii wanaochipukia wanapaswa kusikiliza aina tofauti za muziki ili kupata msukumo wa kutoa muziki mzuri.

Aidha mkali huyo amewashauri kushirikiana na wakongwe wa muziki nchini uganda kwa kuwaheshimu kila wakati badala ya kufikiria kwamba wao ndiyo bora zaidi.

Ikumbukwe Weasel alikuwa na ukaribu sana na msanii redio ambaye walikuwa wakifanya kazi kwa pamoja kwenye good life crew lakini tangu kufariki kwa msaani huyo mashabiki kadhaa wa muziki na wakosoaji nchini Uganda hakuwa na Imani nae lakini mwisho wa siku alifanikiwa kujisamamia kama msanii wa kujitegemea.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa