MSANII WA SOL GENERATION BENSOUL ATAKA BANGI IHALALISHWE NCHINI

You are currently viewing MSANII WA SOL GENERATION BENSOUL ATAKA BANGI IHALALISHWE NCHINI
  • Post category:Burudani

Msanii wa Sol Generation, Bensoul amejiunga rasmi na baadhi ya watu nchini wanaoshinikiza kuhalalisha kwa bangi.

Akipiga stori kwenye kipindi cha Bonga na Jalas, Mkali huyo wa ngoma ya Nairobi amesema kwamba kuhalalisha kwa mmea huo kutasaidia kukuza uchumi wa Kenya.

Aidha ameenda mbali zaidi na kusema kuwa bangi humsaidia kufanya kazi zake kwa umakini bila ya kuchoka.

Bensoul anajiunga na msanii mwenzake Octopizzo pamoja na seneta wa Narok Ledama Olekina ambao wamekuwa wakishinikiza kuhalalishwa kwa bangi nchini

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa