MSANII WA NIGERIA OMAH LAY ADAI BADO ANAPENDA NCHI YA UGANDA.

You are currently viewing MSANII WA NIGERIA OMAH LAY ADAI BADO ANAPENDA NCHI YA UGANDA.
  • Post category:Burudani

Mwanamuziki anayekuja kwa kasi nchini Nigeria Omah Lay amedokeza kuwa yuko tayari kutumbuiza tena nchini Uganda ikiwa atapata nafasi.

Kwenye mahojiano na Redio moja  huko Lagos, nchini Nigeria, hitmaker huyo wa “Bad Influence” amesema anaifanyia kazi albamu yake mpya ambayo inazungumzia tukio la kukamatwa kwake nchini Uganda.

Aidha amethibitisha ikiwa mapromota wa muziki nchini Uganda watazungumza na uongozi wake,hana budi kurudi kutumbuiza nchini humo.

“Sijuti kukamatwa huko Uganda, nilijifunza mengi kutokana na tukio nzima. Natumai nitatumbuiza tena pande hizo, naifanyia kazi albamu yangu mpya ambayo inazungumzia matukio yote yaliyonikuta nchini Uganda,” amesema kwenye mahojiano.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa