MSAJILI WA VYAMA VYA KISIASA KUVIFUTA VYAMA VITAKAVYOLETA FUJO KIPINDI CHA UCHAGUZI

You are currently viewing MSAJILI WA VYAMA VYA KISIASA KUVIFUTA VYAMA VITAKAVYOLETA FUJO KIPINDI CHA UCHAGUZI

Msajili wa Vyama vya Siasa Nchini Anne Nderitu atavifutia usajili Vyama vya Siasa ambavyo shughuli zao zitakumbwa na ghasia kuelekea wakati wanapojiandaa na Uchaguzi Mkuu wa 2022.

Nderitu amevitaka Vyama ambavyo wanachama wao walihusika katika ghasia zilizozikumba Chaguzi ndogo katika maeneo ya Bunge na Wadi kadha wiki jana vijisafishe.

Kulingana na kipengele cha 91 cha Katiba, Vyama vya Siasa havipaswi kuhusishwa au kushiriki katika fujo, kwa kutoa vitisho au kushambulia Wanachama wa Vyama vingine.

Pia, havipaswi kushiriki ufisadi, kupokea au kutumia pesa haramu na kutumia rasilimali za Umma isipokuwa fedha ambazo zimetengewa kupitia hazina ya Vyama vya Siasa.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa