MENEJA WA CHAMELEONE AKANA MADAI YA KUFUTWA KAZI NA MSANII HUYO.

You are currently viewing MENEJA WA CHAMELEONE AKANA MADAI YA KUFUTWA KAZI NA MSANII HUYO.
  • Post category:Burudani

Baada ya uvumi kusambaa mitandoni kuwa  msanii kutoka nchini Uganda Jose Chameleone ana mpango wa kumtimua meneja wake Bijoue Fortunate kwa kuzembea kazini.

Sasa meneja huyo amejitokeza na kunyoosha maelezo kuhusiana na suala hilo kwa kusema kuwa bado anafanya kazi na Jose Chameleone.

Akipiga stori na runinga moja nchini Uganda Fortunate amesema kwamba  kama kweli Chameleone angekuwa na mpango wa kuvunja mkataba wake angefuata taratibu nzuri za kumfikishia taarifa hizo.

Hata hivyo Jose Chameleone bado yupo kimya juu ya suala hilo ila wajuzi wa mambo wanasema kwamba huenda Fortunate akatimulia kama meneja wa msanii huyo baada ya kutofanikisha malengo yake ya kimuziki. 

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa