MBWA WA MSANII WA LADY GAGA WAPATIKANA SALAMA BAADA YA KUIBIWA.

You are currently viewing MBWA WA MSANII WA LADY GAGA WAPATIKANA SALAMA BAADA YA KUIBIWA.
LOS ANGELES, CALIFORNIA - SEPTEMBER 24: Lady Gaga arrives at the Premiere Of Warner Bros. Pictures' 'A Star Is Born' at The Shrine Auditorium on September 24, 2018 in Los Angeles, California. (Photo by Neilson Barnard/Getty Images)
  • Post category:Burudani

Hatimaye Bulldog mbili za Kifaransa za Nyota wa muziki kutoka Nchini Marekani Lady Gaga zimepatikana salama mwishoni mwa juma lilopita baada ya kuibiwa,

Mbwa hao wawili koji na Gustav waliibiwa Jumatano usiku wiki iliyopita baada ya mtu mwenye bunduki kumpiga risasi Ryan Fisher aliyekuwa akiwatembeza mbwa hao huko Los Angeles

Lady Gaga alikuwa ameahidi kutoa shillingi millioni 5.4 kwa mtu yeyote atakayefanikisha kupatikana kwa Bulldogs hao

Kwa mujibu wa Taarifa iliyotolewa na polisi wa Los Angeles mwanamke mmoja ambaye jina lake halijatajwa ndiye aliwapeleka kituoni hapo, na inaonekana mwanamke huyo “hajahusika na hana uhusiano wowote” na shambulio hilo.

Bado Hakuna Taarifa nyingi juu ya jinsi mwanamke huyo aliwapata mbwa hao, lakini hivi karibuni atakuwa tajiri wa shillingi millioni 5.4 kwani Lady Gaga atakuwa amefurahi na kufarijika sana baada ya kupatikana kwa Bulldogs hao.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa