Baada ya Mbosso kutangaza kuwa album yake ya “Definition Of Love” atatoka rasmi siku ya valentines Februari,14, msanii huyo wa bongofleva ametangaza tena tarehe mpya ya kuiachia album hiyo.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram Mbosso amepost picha iliyoandikwa tarehe mpya ya kuiachia album ya “Definition Of Love” ambayo ni Machi 13 mwaka huu bila kuweka sababu za kuisogeza mbele tarehe ya kuiachia album hiyo.
Album ya “Definition Of Love” itakuwa ni album ya kwanza kutoka kwa Mbosso tangu aanze safari yake ya muziki, lakini pia Mbosso atakuwa msanii wa pili kutoka lebo ya WCB kuachia album mwaka huu baada ya rayvanny ambaye aliachia album yake iitwayo “Sound From Africa”.