MAHAKAMA KUU MJINI KITALE YATOA AMRI YA KUSITISHWA KWA SHUGHULI ZOTE ZA SHIRIKA LA NRT KAUNTI YA POKOT MAGHARIBI

You are currently viewing MAHAKAMA KUU MJINI KITALE YATOA AMRI YA KUSITISHWA KWA SHUGHULI ZOTE ZA SHIRIKA LA NRT KAUNTI YA POKOT MAGHARIBI

Mahakama kuu ya Kitale hii leo imeamuru kusitishwa kwa shughuli zozote za kuhifadhi wanyama pori zinazoendeshwa na shirika la kibinafsi la NRT, katika shamba la ekari elfu 250  katika wadi sita za  kaunti ya Pokot Magharibi. 

Akitoa uamuzi huo, Jaji Mwangi Njoroge ametaka upande wa walalamishi na wahojiwa kusubiri uamuzi wa mahakama hiyo mnamo machi 16 ili kuendeleza shughuli katika shamba hilo na kusitisha shughuli za kuwafurusha wakazi kutoka mashamba hayo. 

Wakazi 550 walielekea mahakamani kwa niaba ya ya wakazi alfu 70 kusitisha shughuli hizo kwa vigezo kuwa wananchi wamenyimwa haki kwani hawakuhusishwa kutoa maoni yao kwa shamba hilo kutwaliwa, na shirika la Northern Rangeland Trust chini ya  ufadhili wa umoja wa ulaya, katika shughuli za kuhifadhi mazingira, mifugo, na wanyama pori.

Shirika la NRT lilikua na mkataba wa maelewano kati ya serikali ya kaunti ya pokot magharibi, kutwaa mashamba hayo ya kijamii kwa miaka 10 kuanzia mwaka 2014 hadi 2024 katika wadi za Seker, Lomut, Kasei, Masol, Weiwei na Endugh maeneo bunge ya Sigor na Kacheliba, kaunti ya Pokot Magharibi.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa